Info (Show/Hide)Bara la Afrika lina kila kitu kuanzia ardhi kubwa yenye rutuba, maziwa makubwa, mito, madini, mazao na mbuga za wanyama. Vilevile ni bara la pili kwa ukubwa na inasemekana binadamu wa kwanza aliishi huko. Pia ni bara linaloongoza kwa kupewa misaada na nchi nyingine. Lakini na mambo yote hayo Afrika ni bara linaloshika nafasi ya mwisho kwenye masuala mengi ya maendeleo? Je tatizo ni nini? Utumwa? Ukoloni? Ukoloni mamboleo? Dr. Malima Bundara mwandishi wa kitabu cha “Waafrika Ndivyo Walivyo?” anasema tatizo ni Waafrika wenyewe. Sikiliza zaidi.